Amiri – Maisha Yenye Sanaa

Katika turubai ya maisha, kila uzoefu huchora mstari tofauti. Hakuna anayejua hili zaidi kuliko Amiri kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Yeye ni msanii mwenye kipaji ambaye alikuja Boise mwaka 2016 na amekuwa akiiongezea tasnia ya sanaa na utamaduni ya jiji tangu wakati huo.

Amiri alikuwa na umri wa miaka 12 tu wakati wazazi wake walipofariki dunia. Alipata kimbilio katika kuchora na sanaa, ambayo ilikuwa shughuli yake tangu akiwa mtoto mdogo. Akiwa mtoto, alinza kujishughulisha na sanaa kwa kuchora watu maarufu, mandhari na wanyama. Wazazi wake walipoondoka na mambo yakawa hatari katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, alisafiri hadi kambi ya wakimbizi nchini Botswana mwaka 2002.

Maisha yaliyojaa sanaa

Sanaa ilikuwa sehemu muhimu ya maisha ya Amiri katika kambi, na akashirikiana na wasanii wengine huko na hata kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi (UNHCR) kuonyesha kazi zake katika maonyesho ya sanaa. Kwa kuuza katika maonyesho hayo, aliweza kununua viatu, chakula na nguo. Pia aliwafundisha wengine jinsi ya kupaka rangi na kuchora wakati alipoishi kambini. “Sanaa imeweza kunisaidia kupitia mambo mengi magumu,” anasema. “Imekuwa sehemu kubwa ya maisha yangu na inanisaidia kuchakata changamoto na hisia tofauti.”

Wakati Amiri alipokuwa na umri wa miaka 14, alianza kufanya sanaa ya Batik, ambayo ni njia ya kupaka rangi kwa kutumia nta inayotumika kwenye kitambaa. Mchakato huo, ambao ulianzia India, ni moja ya mitindo anayopenda sanaa ya Amiri. “Michoro na uchoraji wangu huwa na ujumbe kila wakati,” anasema. “Ninapenda kueleza hisia zangu kupitia kazi ninazounda.”

Kama msanii, Amiri amefanya kazi na rangi za akriliki, rangi za mafuta na rangi za maji. Pia anapenda kuchora kuta kubwa (murals). Katika siku zijazo, Amiri angependa kurudi shuleni kujifunza ujuzi mpya wa uchoraji, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuchora nyumba na kabati.

Kufanya nyumba mpya huko Idaho

Leo Amiri anapenda kuishi Boise. “Mji huu ni wenye amani na una hali ya hewa nzuri,” anasema. “Watu ni wazuri sana hapa na una idadi ya watu inayofaa.” Amiri kwa sasa anafanya kazi mbili—moja akiwa mpishi katika uwanja wa ndege na nyingine kwa biashara inayofua vitambaa kwa ajili ya hospitali na hoteli. Anashukuru kwamba EO ilimsaidia kupata gari ambalo hufanya iwe rahisi zaidi kufika kazini.

Amiri ana binti watatu waliozaliwa na kukua walio nchini Tanzania, wenye umri wa miaka 24, 21 na 19. Familia ni muhimu sana kwake na hupeleka fedha kwa binti zake mara kwa mara kuwasaidia kimaisha.

Unaweza kumfuata Amiri na kuona sanaa yake katika Facebook na Instagram.

Habari Husika